Skip to main content

Lecciones fundamentales

Lecciones fundamentales

7. Hadithi za swahili 2

Kunganyira

Adriana Franco Silva

“Kunganyira” ni hadithi iliyotungwa na Haji Gora Haji na ilichapishwa mwaka elfu mbili na nne. Hadithi hii inahusiana na uroho na mambo mabaya ambayo huletwa nao. Hadithi inatokea katika kijiji kinachoitwa “Nipe Nikupe”, jina linaloonyesha kwamba watu wanaoishi huko walikuwa na ukarimu, lakini mhusika mkuu wa hadithi hii, aitwaye Kunganyira, ana tofauti kubwa nao. Hadithi nzima inahusiana na matendo na mawazo mabaya ya Kunganyira, lakini mwishowe yeye anajifunza kwamba uchoyo humletea hasara. Kunganyira siyo mtu mmoja pekee atakayejifunza somo hili. Pia watu wote wasomao hadithi ya Haji wataelewa jambo kwa sababu hiyo ina maadili na mafundisho yenye maana.

Msingi wa kijiji “Nipe Nikupe” ni utaratibu wa kugawiana na huko kila mtu anawajua wanakijiji wengine wote. Kitendo cha kugawiana kinahusishwa na mtazamo wa makundi ya Waafrika wengi, ambapo umma ni muhimu zaidi kuliko ubinafsi. Kwa sababu hii, watu wa kijiji hiki wanagawiana chakula chao. Hivyo, kama mtu asipokuwa na nyama, watu wengine wa jamii watampa anachohitaji. Kitendo hicho kinafanyika kwa ajili ya manufaa ya umma kwa jumla, kwa sababu inadhaniwa kwamba mtu si mtu bila jamii.

Huko zamani “Nipe Nikupe” kilikuwa kidogo sana, kwa hivyo kila mtu alifahamu mahali ambapo wengine walikuwa hawana chakula au walipokuwa wagonjwa. Watu wa kijiji hiki walikuwa wawindaji na wao wote waligawiana wanyama waliowinda ambapo jirani au familia nyingine walihitaji kitoweo. Kunganyira alikuwa mwindaji bila hodari na alikuwa na watoto wengi waliokuwa wanapenda sana nyama na walipigania chakula kama paka wenye njaa, kwa hivyo Kunganyira alitegemea ukarimu wa wanakijiji daima.

Kwa sababu hii, Kunganyira alipenda sana utaratibu wa kugawiana wa kijiji chake, lakini alitaka pia angalikuwa mwindaji mwenye hodari ili awalishe watoto wake. Siku moja alimkamata kanga wa porini na alikuwa anafurahi sana, lakini alianza kuwa na mawazo ya kiroho. Kunganyira hakutaka jirani zake wafahamu kuwa yeye alikuwa amemkamata kanga huyu na kwa hivyo alimwambia mkewe mpango wake wa kumficha kanga na kutogawia kitoweo. Kunganyira alifikiri kwamba hicho sicho kibaya kwa sababu familia yake ilikuwa kubwa sana na angewagawia wenzake wote nyama ya kanga isingetosha ili awalishe watoto wake. Ingawa mawazo yake yanaweza kudhaniwa kuwa halali, ukweli ni kwamba Kunganyira alipatwa na uroho na pia wakati huo alisahau kwamba marafiki zake walikuwa wamemsaidia ili kuwaletea yeye na familia yake chakula kila mara.

Kunganyira alimficha kanga ndani ya kinu. Mkewe alienda dukani na yeye Kunganyira aliamua kuwaambia watu wa “Nipe Nikupe” kwamba utaratibu wa kupeana vitoweo umalizike mara moja. Baada ya Kunganyira kuwaambia hayo wanakijijij walikuwa na uhakika kwamba Kunganyira alikuwa amempata mnyama mkubwa na hakutaka kugawiana nao nyama aliyopata. Wakati huo huo msichana mmoja alienda nyumbani kwa Kunganyira ili akope kinu, lakini kwa vile kulikuwa hakuna mtu aliamua kuingia na kukichukua. Msichana alipojaribu kuchukua kinu hicho, kanga aliruka na kuponyoka. Kwa hivyo Kunganyira aliporudi kanga alikuwa ameshaondoka.

Kunganyira hakuweza kuamini na wasiwasi ilimjaa. Baadaye mkewe alirudi na Kunganyira alimweleza habari baya iliyokuwa imetokea. Mkewe alikuwa na wasiwasi sana kwa sababu alijua kwamba hakuna mtu atakayetaka kuwagawia kitoweo na watoto wake watalala njaa. Kunganyira alisikitika na kuwaomba watu samaha, lakini wanakijiji waliamua kumpa fundisho na hawakugawia kitoweo naye hadi tabia yake ya uhoro ibadilishwe kuwa tabia ya ukarimu.

Wasifu wa Haji Gora Haji

Adriana Gabriela Bañales De León

Haji Gora Haji ni mshairi Mtanzania mwenye maarufu huko nchini Tanzania, hasa katika visiwa vya Zanzibar, lakini Haji ni mwanamuziki, mwandishi na msimulizi wa hadithi na mashairi pia. Haji Gora alizaliwa tarehe kumi, mwezi wa tatu, mwaka elfu moja mia tisa thelathini na tatu kisiwani Tumbatu. Haji alipokuwa na umri wa miaka mitano, familia yake yote naye walihama kuelekea mji wa Zanzibar.

Familia nzima ya Haji ilikuwa kubwa na hawakuwa na pesa nyingi; Haji ana ndugu tano na wandugu wa kambo kumi na moja. Ndivyo haikuwezekana kumlipia Haji elimu yake, kwa hivyo alijifunza hila rasmi ya familia yake yaani: kuvua samaki. Hilo lilimruhusu awe mtaalamu wa bahari. Wakati huo shule za Kurani tu zilikuwa bure, kwa hivyo Haji alipokuwa na umri wa miaka saba alianza elimu yake katika shule ya Kiislamu. Huko alijifunza mashairi ya kidini yaliyoandikwa kwa Kiswahili yaliyofuata mfumo wa jadi wa mashairi ya Kiarabu. Mashairi hiyo yanasifika kwa kufuata mahadhi yanayokuwa makali sana. Kama wanaume wengi katika Afrika ya Mashariki, Haji ana wake zaidi ya mmoja na anao watoto kumi na nne.

Mnamo mwaka elfu moja mia tisa hamsini na tano, Haji alitunga wimbo wake wa kwanza, alipokuwa mwanachama wa kundi la kuimba na kucheza dansi lililogombea katika mashindano ya heshima ya Tumbatu. Kwa hivyo wimbo huo ulikuwa unahusiana na kisiwa cha Tumbatu na uzuri wake. Kuanzia wakati hiyo Haji alijulikana kama msemaji mmoja mkuu wa mashairi na nyimbo katika lugha za Kiswahili na Kitumbatu, ambacho ni lugha ya mama yake. Mashairi yake kadhaa yameshaandikwa katika lugha hizo zote mbili. Mwaka elfu moja mia tisa tisini na nne Haji alichapisha kitabu chake cha mashairi, kinachoitwa Kimbunga. Kutokana na umaarufu wa kitabu hiki Haji alipata umashuhuri mjini Zanzibar na pia kitabu hiki kimetafsiriwa katika Kiingereza, Kifaransa na Kiholanzi.

Ingawa watu wengi wanadhani kwamba shairi la “Kimbunga” linaelezea uharibifu ambao kimbunga kilisababisha, Haji amefafanua kwamba shairi hilo linahusiana na ukatili uliofanyika katika mapinduzi ya Zanzibar mnamo mwaka elfu moja mia tisa sitini na nne. Kwa njia ya kutumia mafumbo, shairi hili linakitaja Chama cha Afro-Shirazi1 na Ushirikiano wa Tanganyika wa Umoja wa Kitaifa. Pia linamkumbusha msomaji historia kuhusu Zanzibar na mabadiliko yote ambayo mapinduzi yalisababisha katika maisha ya wananchi wa kisiwa hiki (Lichtenstein 2012).

Mwaka elfu mbili na tisa Haji alichapisa kitabu chake cha pili, kinachoitwa Siri ya Gining’i. Pia Haji alishiriki katika tamasha za mashairi katika miji kadhaa, kwa mfano mjini Medellin nchini Colombia na mjini Rotterdam huko Uholanzi. Mara kwa mara Haji amechangia katika vipindi vya maandishi katika redio ya Tanzania na pia yeye ni mwanachama wa kamati za lugha ya Kiswahili (Samsom 2002). Vilevile Haji anafurahia kusoma mashairi ya waandishi wengine kutoka nchi mbalimbali.

Sasa, mashairi na hadithi ya Haji Gora hutumika shuleni Tanzania, lakini hajapata faida nyingi kwa maandiko yake ambayo yamechapishwa; Haji amesema kwamba ameshapata dola mia mbili tu (Lichtenstein 2012). Kwa vyovyote yeye ameamua kwamba hataacha kutunga mashairi kamwe. Haji amejitolea zaidi ya miaka arobaini kwa kuandika fasihi simulizi, mashairi na hadithi na inaonekana hakuna kitu kinachoweza kumsababisha aache.

Marejeo


1Chama cha Afro-Shirazi (ASP, akronimi katika Kiingereza) kilikuwa muungano wa vyama vya Shirazi na vyama vya Waafrika vilivyokuwa Zanzibar. Wakati wa mapinduzi ya Zanzibar, ASP pamoja na Ushirikiano wa Tanganyika Wa Umoja wa Kitaifa (TANU, akronimi katika Kiingereza) waliangusha serikali ya Waarabu ilioongozwa wa Jamshid bin Abdullah na waliumba Jamhuri ya Watu wa Zanzibar. Baada ya miezi michache, Jamhuri hii iliungana na Tanganyika ili kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ujamaa

Javier Sacristán de Alva

Tanganyika. Ili afanye hivyo Nyerere alitaka kilimo kiwe kitendo kikuu cha uchumi wa nchi. Mambo hayo yalikuwa magumu ili yafanyike. Mpango wa vijiji vya ujamaa vya Tanganyika ulikuwa viwe kama kijiji cha hadithi hiyo kinachoitwa “Nipe Nikupe”.

Rais wa Tanganyika alitaka nchi yake ianze kuongeza mazao yake ya kilimo. Kwa hivyo mnamo mwaka elfu moja mia tisa sitini na saba aliandika Azimio la Arusha1 ili apange Tanzania jinsi itakavyokuwa katika wakati ujao. Azimio la Arusha lilieleza siasa ya ujamaa, huko likisema kwamba mali ya mashamba yatabadilika yawe mali ya wakulima wote wa kila kijiji.

Serikali ya Tanzania ilijikuta na mapinzano makubwa kwa sababu katika utamaduni wa Watanzania kwa ujumla kulikuwa na sehemu mbili tu, Rungwe na Sumbawanga, ambapo waliishi katika vijiji vilivyofanana na vijiji vya ujamaa2. Kwa hivyo, kujenga vijiji kulikuwa muhimu mno katika wakati wa ujamaa kwa sababu mahala ya mashamba yalikuwa mbali na hapakuwa rahisi kuendeleza kilimo katika sehemu hizi zote3. Ujamaa ulikuwa umefuatia wazo ya Rungwe na Sumbawanga lakini wakulima hawakubadili kwa haraka na wengine hawakutaka kubadili moja kwa moja.

Nyerere alitaka kujenga vijiji kwa sababu Tanzania ilihitaji pesa zitokazo nchi zingine ili kupata teknolojia bora ya kilimo na kadhalika. Mpango wa ujamaa ulitegemea sana wakulima wa Tanzania kwa sababu serikali ilitaka iwaongoze wakulima lakini bila kuwaambia wafanyeje moja kwa moja4.

Wanahistoria wengi wanasema kwamba uchumi ni ujuzi uliotoka kwa watu waliojifunza nje ya Afrika. Uchumi wa wakati kabla ya Wazungu kufika Afrika ulikuwa kama ule wa kijiji cha “Nipe Nikupe.” Wazungu walipoanza ubepari na Waafrika walianza kujifikiria wao wenyewe tu. Nyerere alidhani kwamba kulikuwa lazima Watanzania wafanye kazi pamoja kama zamani5.

Nyerere alitaka Watanzania wenye adabu kwa hivyo Kiswahili kilianza kutumika shuleni, pia alifanya bidii ili wakulima wawe na shule za sekondari. Walimu wa mashule hayo walifundisha maarifa ya kilimo kwa sababu shule zilikuwa zinafuata maarifa ya Chama cha Mapinduzi6.

Ujamaa ulianza kuwa na matatizo mengi mnamo mwaka elfu moja mia tisa sabini na tano. Mwaka huu kulikuwa na njaa Tanzania kwa hivyo ilikuwa lazima kuingiza tani elfu ishirini na tano ya mahindi nchini kutoka nchi za nje7. Njaa ilisababisha watu wengi wawe kama Kunganyira baada ya kumpata kanga wake.

Serikali ya Tanzania ilijaribu kubadili uhusiano kati ya wakulima, kazi za kulima na mazao nchini Tanzania lakini haikuweza kufanya hivyo isipokuwa mara chache. Mara nyingi Ujamaa haukufikia hatua ya mwisho katika maendeleo yake lakini kuna vijiji vilivyokuwa na duka la kijiji au shamba kubwa ili watu wawe na kazi, ijapokuwa mali ya binafsi bado ilikuwa chango la kawaida sana. Ujamaa haukuwa na mafanikio hasa kwa sababu wakulima walitaka pesa na walikuwa kama Kunganyira.

Haji Gora Haji alimtumia mhusika wa Kunganyira ili aonyeshe hasara ya ukoloni, kwa sababu yeye aliacha kuwafikiria majirani wake na sasa alijifikiria mwenyewe tu. Ni lazima msomaji aone kwamba watu wote wanaoishi katika hali ya ujamaa ni lazima wakumbuke jina la kijiji cha hadithi hiyo “Nipe Nikupe.”

Marejeo

  • Ergas, Zaki, “Why Did the Ujamaa Village Policy Fail? – Towards a Global Analysis”, The Journal of Modern African Studies, Vol. 18, No. 3 Mwezi wa tisa, 1980, p. 387-410, katika http://www.jstor.org/stable/720947
  • Kjekshus, Helge, ”The Tanzanian Villagization Policy: Implementational Lessons and Ecological Dimensions”, Canadian Journal of African Studies / Revue Canadienne des Études Africaines, Vol. 11, No. 2, 1977, pp.269-282, katika http://www.jstor.org/stable/483624
  • Mohiddin, Ahmed, “Ujamaa: A Commentary on President Nyerere’s Vision of Tanzanian Society”, African Affairs, Vol.67, No. 267, Mwezi wa nne, 1968, p. 130-143, katika http://www.jstor.org/stable/720947

1Helge Kjekshus, ”The Tanzanian Villagization Policy: Implementational Lessons and Ecological Dimensions”, Canadian Journal of African Studies / Revue Canadienne des Études Africaines,Vol. 11, No. 2, 1977, p.269, katika http://www.jstor.org/stable/483624

2Ibid. p. 271

3Ibid. p. 273

4Ibid. p. 275

5Ahmed Mohiddin, “Ujamaa: A Commentary on President Nyerere’s Vision of Tanzanian Society”, African Affairs, Vol.67, No. 267, Mwezi wa nne, 1968, p. 134, katika http://www.jstor.org/stable/720947

6Zaki Ergas, “Why Did the Ujamaa Village Policy Fail? – Towards a Global Analysis”, The Journal of Modern African Studies, Vol. 18, No. 3 Mwezi wa tisa, 1980, p. 390, katika http://www.jstor.org/stable/720947

7Ibid. p. 392